Thursday, June 6, 2013

United bado ina ndoto ya kumrejesha Cristiano Ronaldo Old Trafford

Bado kuna tetesi kuwa uongozi ya Manchester United una matumaini ya kumrudisha mshambuliaji wao wa zamani Cristiano Ronaldo ambaye alisajiliwa na Real Madrid kutoka kwao kwa ada ya uhamisho wa €94 million.

Kwa mujibu wa mtandao wa Sportmail, CEO David Gill wa Manchester United ameongea na wakala wa Ronaldo kuhusu kurudi Old Trafford ili kukisaidia kikosi hicho katika ligi kuu ya Uingereza na ligi ya mabingwa wa Ulaya.
Kumekuwepo na etesi endapo Ronaldo atarejea Old Trafford kuna uwezekano mkubwa wa Wayne Rooney kuendelea kucheza soka United. Hivi karibuni kumekuwepo na habari kuwa Wayne Rooney anawindwa na club mbalimbali ikiwemo Chelsea waliokwisha tangaza dau la £25m

0 comments:

Post a Comment