This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Saturday, June 24, 2017

LUKAKU IN TANZANIA SOMA HAPA UJUE ZAIDI


Hakika hili ni swali ambalo kila mmoja wetu kwa sasa analiwaza akifikiria ujio wa klabu ya Everton ambao watakuja Tanzania mapema mwezi ujao.
Tayari ilishathibitishwa kwamba Lukaku hatakuwa na Everton katika msimu ujao wa ligi lakini hadi sasa Mbelgiji huyo hajasajiliwa na klabu yoyote ile.
Chelsea walitajwa kuongoza mbio za kumnunua Lukaku na tetesi zilisema wanakaribia kumsaini mshambuliaji huyo kwa dau la euro 100m lakini hadi sasa suala hilo limetawaliwa na ukimya.
Baadae Manchester United nao walionekana kuhamia kwa Lukaku baada ya uhamisho wa Antoine Griezman kushindikana lakini nao pia kama ilivyo kwa Chelsea hadi sasa hawajamsaini.
Inafahamika kwamba kikwazo kikubwa kumnunua Lukaku ni dau lake ambalo linakadiriwa sio chini ya euro 90 million, pesa zinazooenekana ni nyingi.
Manchester United wanamhitaji Lukaku kuziba nafasi ya Zlatan Ibrahimovich, Chelsea nao wanamuhitaji kuziba nafasi ya Diego Costa lakini hadi sasa wote wanaonekana kutoeleweka.
Bado wiki chache tu kampuni ya Sport Pesa iwalete Everton na watu wengi wanamsubiri Lukaku kuona kama atakuja au laa, hakika hili limatufanya kuvuta subira hadi siku hiyo Sport Pesa watakapowaleta Everton pale Temeke uwanja wa taifa.

DEAL DONE: majogoo wa London klabu ya Liverpool walithibitisha kumsajili winga wa As Roma

Jana majogoo wa London klabu ya Liverpool walithibitisha kumsajili winga wa As Roma Mohed Salah ambaye walimtafuta kwa muda sasa kwa dau la euro million 39. Hii sio mara ya kwanza kwa Salah kucheza katika ligi kuu nchini Uingereza kwani hapo mwanzo kabla hajahamia nchini Italia aliwahi kukipiga na timu ya Chelsea. Mohamed Salah amesema ujio wake Liverpool ni tofauti na Chelsea kwani kipindi wakati anaenda Chelsea alikuwa bado mtotomtoto lakini sasa anajiona ni bora zaidi. “Nina uhakika 100% kwamba kila kitu kimebadilika hadi muonekano wangu,kipindi kile nilikuwa na miaka 20 ila sasa nina 24 na nina uzoefu mkubwa zaidi tofauti na hapo mwanzo” alisema Salah. Mkataba wa Salah na Liverpool utamfanyia kila mwisho wa wiki kuweka kiasi cha euro 90,000 huku akikabidhiwa jezi namba 11 na Firminho akipewa jezi namba 9. Usajili wa Mohamed Salah wa euro million 39 umevunja rekodi ya usajili ya klabu hiyo ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Andy Caroll aliyesajiliwa kwa euro milion 35 mwaka 2011.Na hii ndio orodha ya usajili wa ghali ndani ya klabu hiyo. 1.Mohamed Salah (euro 39m). 2.Andy Carroll (euro 35m). 3.Sadio Mane (euro 34m) 4.Christian Benteke (euro 32.5m) 5.Roberto Firminho (euro 29m) Comments 0 comments SHARE Facebook Twitter Previous articleWanyama na siri ya jezi namba 67 mgongoni Next articleLioneil Messi na baba yake wafanikiwa kuikwepa jela Kicki_19 http://www.shaffihdauda.co.tz RELATED ARTICLESMORE FROM AUTHOR Manchester United na Nemanja Matic bado kidogo tu Edin Dzeko anaamini mchezaji huyu ndio bora zaidi kuwahi kucheza naye Lioneil Messi na baba yake wafanikiwa kuikwepa jela LEAVE A REPLY

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI 24.06.2017 HIZI HAPA CLICK USOME WHATS HAPENING

Arsenal wamekuwa na mazungumzo zaidi na Lyon kuhusu mshambuliaji Alexander Lacazette, 26, ambaye huenda akasajiliwa kwa kuvunja rekodi ya Arsenal, kwa pauni milioni 49 (Telegraph). Arsenal wanajiandaa kulipa euro milioni 60 ili kumsajili Alexandre Lacazette kutoka Lyon. Lacazette alikuwa anakaribia kuhamia Atletico Madrid kabla ya timu hiyo kufungiwa kusajili (L’Equipe). Chelsea wamekubaliana kimsingi na Monaco kumsajili kiungo Tiemoue Bakayoko, 22, na wana matumaini ya kukamilisha uhamisho huo wa pauni milioni 35.1 wiki ijayo (Evening Standard). Manchester United wanapiga hatua katika kumfuatilia mashambuliaji Alvaro Morata, 24, lakini bado hawajakubaliana ada ya uhamisho na Real Madrid (ESPN). Liverpool watapanda dau jingine kumtaka Kylian Mbappe, 18, ikiwa wanaamini kuwa kweli mshambuliaji huyo anataka kuhamia Uingereza (Times). Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amezungumza na Kylian Mbappe na kujadili uhamisho wake kwenda Emirates na pia mipango ya mbele ya uchezaji wake (L’Equipe). Meneja wa Real Madrid Zinedine Zidane amemuambia Kylian Mbappe kuwa atauza mmoja wa washambuliaji wake ikiwa mchezaji huyo atakubali kuhamia kwa mabingwa hao wa Ulaya (L’Equipe). Arsenal wapo tayari kumuuza Alex Oxlade-Chamberlain, 23, huku Liverpool wakimtaka mchezaji huyo, ambaye huenda akawa miongoni mwa wachezaji saba watakaouzwa na Arsenal msimu huu (Independent). Newcastle wanakaribia kukamilisha mkataba wa pauni milioni 8.7 kumsajili beki wa Eibar, Florian Lejuene 26 (Evening Chronicle). Bayern Munich wanataka kumsajili winga wa Atletivo Madrid Yannick Carrasco, 23, ambaye anauzwa kwa pauni milioni 43 (AS). Mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney, 31, anashindwa kupata klabu ya kwenda kwa kuwa timu nyingi hazipo tayari kulipa mshahara wake mkubwa pamoja na ada ya uhamisho (Mirror). Manchester United wametupilia mbali tetesi kuwa Nemanja Matic amefikia makubaliano ya maslahi binafsi kuhamia Old Trafford (Daily Telegraph). Manchester United wametoa dau la euro milioni 70 kumtaka beki wa Paris Saint-Germain Marquinhos (Globo Esporte). Ousmane Dembele anataka kuondoka Borussia Dortmund kufuatia kufukuzwa kazi kwa meneja Thomas Tuchel. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa hataki kwenda Barcelona, lakini Chelsea na Manchester United zinamfuatilia (Eurosport). Stoke City wameionya Arsenal kutomfuatilia kipa wake Jack Butland, 24 (Stoke Sentinel). Manchester City wanasisitiza kuweka kipengele cha kumnunua tena Kelechi Iheanacho, 20, kwenye mkataba wake wa mauzo, huku Leicester City na West ham wakimtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Nigeria (Telegraph). Manchester United wanamtaka beki wa kushoto wa Barcelona Jordi Alba, 28, lakini itakuwa vigumu kumpata msimu huu (ESPN). Winga wa Everton Gerard Deulofeu, 23, anasakwa na Roma (Romanews). Huddersfield, waliopanda daraja msimu huu EPL, wanajiandaa kulipa pauni milioni 11.5 kumsajili mshambuliaji wa Montpellier Steve Mounie 22 (Mirror). Galatasaray wamepanda dau la kumtaka kiungo wa Chelsea Mario Pasalic, 22, ambaye alihamia darajani mwaka 2014 lakini hajawahi kucheza (Miliyet). Barcelona wana matumaini kuwa huenda wakafikia makubaliano ya kumsajili Ousmane Dembele, 20, kutoka Borussia Dortmund msimu ujao (Mundo). Brighton watamfuatilia kiungo wa Middlesbrough Stewart Downing, 32, ambaye ameambiwa na meneja wake Garry Monk kuwa anaweza kuondoka Riverside (Sun). Manchester United wamepata matumaini ya kuweza kumsajili Renato Sanches kutoka Bayern Munich, baada ya timu hiyo ya Ujerumani kumsajili Corentin Tolisso (The Sun). Tottenham wanajiandaa kutoa dau la pauni milioni 17.5 kumsajili kiungo wa Schalke Max Meyer (The Sun) Bayern Munich sasa wanaelekeza juhudi zao kumsajili Yannick Ferreira Carrasco, baada ya kupunguza kasi ya kutaka kumsajili Alexis Sanchez kutoka Arsenal (L’Equipe). Chelsea wanakaribia kumsajili beki wa kati wa Southampton Virgil va Dijk kwa pauni milioni 60 (Sky Italia). Kiungo wa Monaco Fabinho, 23, atagharimu euro milioni 45. Juventus, Manchester United, Manchester City na Paris Saint-Germain wanamtaka mchezaji huyo kutoka Brazil (Calcio Mercato). Manchester United wanamnyatia beki wa Barcelona Jordi Alba (ESPN). Dau la pauni milioni 31 la Manchester United kumtaka Andre Gomes limekataliwa na Barcelona (Catalunya Radio). Tottenham wanataka kumsajili kiungo wa AC Milan Suso (Marca). Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Weekend Njema nyote!!

QUICK ROCKA NA OMG WANAYO KICHUPA HIKI KWA AJILI YAKO "WATASEMA" CLIP IANGALIE HAPA


Baada ya crew ya OMG kufanya poa na video yao “Uongo na Umbea” hapa wamekutana tena na boss wao, Quick Rocka mmiliki wa studio za Switch Records ambazo OMG wamesaini kufanya kazi chini ya lebel hiyo. Leo wameachia video yao mpya “Watasema” ambayo kuna sehemu wamesample wimbo wa TID “Watasema Sana”
.

MUONEKANO WA NYUMBA YA LIL WAYNE ALIO UPIGA BEI PICHA ZA NYUMBA MUONEKANO WA NJE NA NDANI HUU HAPA




Mastaa mbalimbali duniani hupenda siyo tu kununua na kuendesha magari ya kifahari pia wako mstari wa mbele kununua nyumba za nguvu lakini hawapendi kuzitumia kwa muda mrefu.

Story iliyonifikia ni kuhusu kupatikana mmiliki mpya wa jumba la kifahari lililopo Miami Beach, Fla. ambalo lilikuwa milki ya Rapper Dwayne Michael Carter Jr., maarufu kama Lil Wayne ambaye ameliuza kwa Dollar 10m ambazo ni zaidi ya Tsh. 22b.

Mjengo huo awali uliingia sokoni mwaka 2015 kwa bei ya Dollar 18m zaidi ya Tsh. 39.6b lakini likakosa mnunuzi na likashushwa bei hadi Dollar 12m zaidi ya Tsh. 26.4b hakupatikana pia mteja kabla ya kuuzwa kwa bei hiyo.

Nimekuwekea hapa za muonekano wa ndani na nje ya jengo hilo.

Friday, June 23, 2017

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 23.06.2017 NA MAGAZETI MJINI LONDON SOMA HAPA ZAID

Paris-Saint Germain wapo tayari kutoa kitita kitakachovunja rekodi ya dunia cha pauni milioni 119 kumsajili Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco (Mirror). Lakini Arsenal wanajiandaa kutoa dau jipya kumsajili Mbappe, huku Arsene Wenger akiwa na uhakika wa kumpata mchezaji huyo (Metro). Mbappe hana tatizo la wazo la kwenda Emirates (Telegraph). Dau la pauni milioni 100 kutoka Liverpool la kumtaka Kylian Mbappe limekataliwa (Marca). Mbappe inasemekana amekuwa na mazungumzo na meneja wa Real Madrid Zinedine Zidane (L’Equipe). Meneja wa Chelsea Antonio Conte yuko tayari kumuuza kiungo Nemanja Matic, 28, kwenda Manchester United ili aweze kufanikisha usajili wa kiungo wa Monaco Tiemoue Bakayoko, 22, kwa pauni milioni 42 (The Times). Real Spciedad wamekubali kulipa pauni milioni 10 kumsajili winga wa Manchester United Adnan Januzaj, 22 (Daily Mail). Beki Matteo Darmian wa Manchester United amempigia simu Jose Mourinho na kumuomba amsaidie katika kuhamia Juventus (Sun). Mwenyekiti wa Stoke City Peter Coates amesisitiza kuwa hana mipango ya kumuuza Xherdan Shaqiri, 25, msimu huu (TalkSport). Dau la pauni milioni 12 la Stoke kumtaka beki wa Middlesbrough Ben Gibson, 20, limekataliwa. Middlesbrough wanataka zaidi ya pauni milioni 20 (Mirror). Tottenham wamewasiliana na Fiorentina, kumuulizia kiungo Matias Vecino, 25 (TalkSport). Tottenham wapo tayari kutoa pauni milioni 17.5 kumsajili winga wa Schalke Max Meyer (Sun). Spurs pia wanajiandaa kumpa mkataba mpya wa miaka mitano beki wa kulia Kieran Trippier, 26, (Mirror). Liverpool wameambiwa na Borussia Dortmund kuwa mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang, 28, atagharimu pauni milioni 63 (Bild). Liverpool wamekataa dau la pauni milioni 11 kutoka Napoli la kumtaka beki Alberto Moreno 24 (Telegraph). John Terry anafikiria kwenda Aston Villa, huku akitarajia timu nyingine za Ligi Kuu zitamtaka pia (Guardian). Antonio Conte amewaambia Chelsea kuwa anamtaka Leonardo Bonucci, 30, wa Juventus au Virgil van Dijk, 25 wa Southampton ili kuimarisha safu yake ya ulinzi (Guardian). Burnley wana matumaini ya kuwakatisha tamaa West Brom katika mbio za kumsajili beki wa kushoto wa Leeds Charlie Taylor, 23 (Burnley Express). Bayern Munich wapo tayari kumtoa kwa mkopo winga wa zamani wa Arsenal Serge Gnabry, baada ya kumsajili msimu huu, huku wakisaka jina kubwa katika ushambuliaji (SportBild). Lyon wamekubaliana ada ya pauni milioni 16.7 kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Bertrand Traore, 21 (L”Equipe). Intare Milan wanafikiria kupambana na Juventus katika kumsajili kipa wa Arsenal Wojciech Szczesny, 28 (Evening Standard). Chelsea wanakaribia kukamilisha usajili wa pauni milioni 100 wa Leonardo Bonucci na Alex Sandro kutoka Juventus (The Sun). Manchester City wanazidi kuamini kuwa wataweza kumsajili Alexis Sanchez, 28, kwa pauni milioni 50. Chelsea nao wanataka kujaribu kupanda dau kumchukua Sanchez na watatoa dau rasmi hivi karibuni (Daily Mirror). Arsenal wanataka kumfanya Jack Butland kuwa mrithi wa Petr Cech (Daily Star). Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Weekend Njema nyote!!

Ben Pol ft Darassa - Tatu (Official Music Video )

Gumzo lake lilianzia baada ya kufuta picha zote kwenye Instagram yake na kisha kupost picha chache akiwa bila nguo na mwili wake ukionekana umeng’aa baada ya kupakwa mafuta ambapo alipoulizwa alisema ni wimbo mpya unakuja unaitwa ‘tatu‘

Iangalie hapa

Friday, February 17, 2017

Paul Pogba vs Florentin Pogba, Zlatan kamsaidia Paul kumfunga kaka yake



Usiku wa February 16 ulikuwa ni usiku wa kihistoria katika familia ya mchezaji ghali zaidi dunia Paul Pogba ambapo kwa mara ya kwanza aliingia uwanjani katika mchezo wa UEFA Europa League kucheza dhidi ya kaka yake wa damu Florentin Pogba ndani ya uwanja wa Old Trafford.


Huu ni mchezo ambao Paul Pogba alikuwa akiichezea Man United wakati Florentin Pogba akiichezea St Etienne, kivutio cha mchezo huo kilikuwa ni kwa mama na kaka wa ndugu hao Mathias Pogba ambaye aliamua kutengeneza jezi maalum nusu St Etienne na nusu Man United kuonesha upendo kwa ndugu zake wote bila upendeleo.



Katika game hiyo Man United walifanikiwa kupata ushindi wa goli 3-0, shukrani pekee ziende kwa Zlatan Ibrahimovic aliyepiga hat-trick katika game hiyo, wakati Paul Pogba akiishia kugongesha post dakika ya 69 ya mchezo, magoli ya Zlatan yanamfanya aweke rekodi ya kuifunga St Etienne kwa mara ya 17 katika michezo 14 aliyocheza dhidi yake.


Paul Pogba na Florentin Pogba Kwa upande wa familia ya Pogba ambapo Mourinho siku moja kabla ya game alisema kuwa anajua mama yao na Pogba ataomba game iishe kwa sare, ameshuhudia mtoto wake mmoja akiondoka na furaha mwingine majonzi, kama ufahamu Paul Pogba ana makaka wawil ambao pia wanacheza soka na ni mapacha Florentin Pogba aliyecheza dhidi yake leo na Mathias Pogba anayecheza Sparta
ebu angalia na hii apa

Wednesday, February 15, 2017

Friday, February 3, 2017

BREAKING: Rais Magufuli kateua Mkuu mpya wa Majeshi Tanzania anaechukua nafasi ya Mwamunyange


 IKULU Dar es salaam ambapo Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amefanya utauzi wa Mkuu mpya wa majeshi ya ulinzi na usalama Tanzania kama inavyosomeka kwenye hii taarifa hapa chini.

Aliyeteuliwa kuchukua nafasi ya Davis Mwamunyange ni Venance S. Mabeyo ambapo pamoja na kuteuliwakuwa mkuu wa majeshi ya ulinzi Tanzania Mabeyo amepandishwa cheo na kuwa Jenerali.

Jenerali Venance anachukua nafasi ya Jenerali Davis Mwamunyange ambaye amestaafu ambapo kitu kingine cha kufahamu ni kwamba Rais Magufuli amemteua Meja Jenerali James M. Mwakibolwa kuwa Mnadhimu mkuu wa majeshi ya ulinzi Tanzania.

Pamoja na kuteuliwa kuwa Mnadhimu mkuu wa Majeshi ya ulinzi Tanzania, Meja Jenerali James Mwakibolwa amepandishwa cheo na kuwa Luteni Jenerali ambapo anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jenerali Venance aliyeteuliwa kuwa mkuu wa majeshi.

Uteuzi huu unaanza mara moja ambapo tarehe ya kuapishwa itatangazwa baadae.