Sunday, January 19, 2014

KUHUSU KIFO CHA Mtangazaji wa BBC TV, Komla Dumor KUFARIKI DUNIA HAPO JANA









Mtangazaji wa BBC TV, Komla Dumor amefariki dunia ghafla jana akiwa nyumbani kwake mjini London, Uingereza.Alikuwa na umri wa miaka 41.


Komla-Dumor


Dumor aliyezaliwa nchini Ghana alikuwa mtangazaji wa BBC World News na aliendesha kipindi cha Focus on Africa.


Mtangazaji huyo alijiunga na BBC kama mtangazaji wa radio mwaka 2007 baada ya kufanya kazi ya uandishi wa habari kwa zaidi ya muongo mmoja nchini Ghana. Rais wa Ghana, John Dramani Mahama aliandika kwenye mtandao wa Twitter kuwa nchi yake imepoteza mmoja wa mabalozi wake muhimu.


Our nation has lost one of its finest ambassadors. @BBCkomladumor was a broadcaster of exceptional quality and Ghana's gift to the world.


— John Dramani Mahama (@JDMahama) January 18, 2014


Inadai kuwa alifariki kwa mshtuko wa moyo.

0 comments:

Post a Comment