Saturday, August 3, 2013

Mfahamu Refa aliyepungua uzito baada ya kupondwa na Sir Alex Ferguson.


.
image
Refa wa mechi za ligi kuu ya England Phil Dowd amejibu kwa vitendo shutuma zilizoelekezwa kwake kwa uzito aliokuwa nao baada ya kurudi kwa ajili ya msimu mpya akiwa amepungua uzito .
Dowd ambaye alikuwa na kitambi ambacho wakati mwingine kilikuwa kinamfanya ashindwe kukimbia wakati wa mechi kubwa alijiandikisha kwenye gym ambayo amekuwa akifanya mazoezi kwa miezi miwili ambapo amefanikiwa kupungua uzito na kuonekana mwembamba .
Huu ndio muonekano mpya wa mwamuzi Phil Dowd baada ya miezi miwili ya mazoezi.
Huu ndio muonekano mpya wa mwamuzi Phil Dowd baada ya miezi miwili ya mazoezi.
Kocha wa zamani wa  Manchester United Sir Alex Ferguson ambaye amezoeleka kwa tabia yake ya kuwashutumu waamuzi pale ambapo timu yake isipofanya vizuri alizungumzia suala la uzito wa refa Phil Dowd baada ya mchezo baina ya Manchester United na Arsenal uliochezwa mwezi aprili mwaka huu baada ya Refa huyo kuwaonyesha wachezaji watano wa United kadi ya njano. Ferguson alisikika akisema kuwa ” refa huyu hakuweza kuendana na kasi ya mchezo na alikuwa anatoa kadi kila anapoona tukio limetokea”.
Cheki kitambi kilivokuwa kabla ya mazoezi .
Cheki kitambi kilivokuwa kabla ya mazoezi .
Phil Dowd aliwahi kushindwa kufikia viwango stahiki vya afya kabla ya msimu uliopita ambapo alilazimika kufanya mazoezi na kupunguza uzito kala yakuruhusiwa kuamua mechi za Epl Na mara zote amekuwa akitukanwa na mashabiki kwa jinsi muonekano wake ulivyo na alivyokuwa anapata tabu kukimbizana na wachezaji huku akiwa anaonekana amechoka

0 comments:

Post a Comment